Breaking News
Loading...

Advert

MICHEZO

MICHEZO

BURUDANI

BURUDANI

SIASA & JAMII KWA UJUMLA

SIASA & JAMII KWA UJUMLA

Recent Post

Monday, May 23, 2016
Wanafunzi walioacha shule kwa ujauzito,kuozeshwa na wazazi wao waamuriwa kurudi shule.soma zaid.

Wanafunzi walioacha shule kwa ujauzito,kuozeshwa na wazazi wao waamuriwa kurudi shule.soma zaid.

Wanafunzi wote walioacha shule
kutokana na kupata ujauzito,utoro,kuozeshwa na
wazazi wameamriwa na Mkuu wa Mkoa wa
Tabora Aggrey Mwanri kurudi shule mara
moja,nakusema kuwa waliowaoa ama kuwapa
ujauzito watajulikana mbele ya safari sheria
zitakapo anza kuchukua mkondo wake

Sunday, May 22, 2016
Rais obama amewasili nchini vietnam hii ni hatua ya kuondoa uhasama kati ya marekani na vietnam.soma zai.

Rais obama amewasili nchini vietnam hii ni hatua ya kuondoa uhasama kati ya marekani na vietnam.soma zai.

Rais wa Marekani Barack Obama amewasili
nchini Vietnam wakati anaanza ziara ya wiki
moja barani Asia.
Maafisa nchini Marekani wanasema kuwa ziara
hiyo ina lengo la kuboresha ushirikiano wa ulinzi
na kiuchumi kati ya mataifa hayo ambayo ni
mahasimu wa zamani.
Waandishi wa habari wanasema kuwa Marekani
inataka kuiunga mkono Vietman na mataifa ya
kusini mashariki mwa Asia yaliyo kwenye mzozo
wa kikanda na China.
Vietnam inaripotiwa kutaka iondolewe vikwazo
vya silaha ilivyowekewa na Marekani.

Madawati yawakosesha usingizi  ma' DC na RC.soma zaid.

Madawati yawakosesha usingizi ma' DC na RC.soma zaid.

VIONGOZI wa serikali hususan wakuu wa mikoa
na wilaya, wako katika heka heka za kutekeleza
kutengeneza madawati. Lengo ni kuhakikisha
hakuna mwanafunzi atakayekaa sakafuni, kabla
ya muda wa ukomo, waliopewa Rais John
Magufuli .
Wakati zikiwa zimebaki siku 39 kabla ya muda
huo wa ukomo ambao ni Juni 30 mwaka huu,
miongoni mwa maeneo ambayo gazeti hili
limefanya ufuatiliaji, imeshuhudiwa mikakati
mbalimbali ikitumika kwa ajili ya kupata fedha za
utekelezaji wa agizo ikiwamo kuangukia
wahisani.
Baadhi ya wakuu wa mikoa wameelekeza
halmashauri zao, kuhakikisha mapato ya vyanzo
vya ndani yanaelekezwa kwenye utengenezaji wa
madawati huku wengine wakishawishi wananchi
kuchangia kwa hiari kutekeleza agizo.
Hata hivyo, katika mchakato huo wa kutekeleza
matakwa ya agizo, baadhi ya maeneo
yamebainika kufanya uchakachuaji kwa
kutengeneza madawati kwa kutumia mabanzi
badala ya mbao ambao hata hivyo, umeshtukiwa
na viongozi wa serikali wa maeneo husika.
Uchakachuaji Vitendo vya matumizi ya mabanzi
badala ya mbao kutengeneza madawati,
vimebainika mkoani Tabora, ambako Mkuu wa
Mkoa, Aggrey Mwanri amebaini hilo na kuagiza
halmashauri zote zenye kufanya hivyo kuacha
mara moja.
Mwanri alibaini hayo hivi karibuni, alipofanya
ziara katika wilaya za Igunga na Nzega, ambako
aliagiza viongozi kufuatilia na kuhakikisha fundi
yeyote atakayebainika kutengeneza madawati
kwa kutumia mabanzi, asilipwe fedha.
Mwanri alisema ni jambo la aibu, kuona madawati
yakitengenezwa kwa mabanzi wakati mbao zipo.
Aliahidi kurudi wilayani Igunga na Nzega, kupiga
kambi kuhakikisha utengenezaji madawati
unakamilika muda uliopangwa.
Aidha aliagiza Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri
ya wilaya ya Igunga, Alois Kaziyaleli kuhakikisha
fedha zote zitokanazo na makusanyo ya vyanzo
vya halmashauri, zinapelekwa katika utengenezaji
wa madawati. Mkuu wa Wilaya ya Igunga,
Zipporah Pangani, Mwenyekiti wa Halmashauri,
Peter Onesmo na Mkuu wa Wilaya ya Nzega,
Jackilin Liana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya
Mji Mdogo wa Igunga, Jeremia Jomanga kwa
nyakati tofauti, walimhakikishia Mwanri kuwa
ifikapo Mei 30, watakuwa wamekamilisha
utengenezaji madawati katika shule zote za
wilaya ya Igunga.
Kulingana na taarifa ya Mwenyekiti wa
Halmashauri ya Wilaya ya Nzega iliyotolewa
kwenye kikao cha Baraza la Madiwani,
Halmashauri imeidhinisha Sh milioni 100 kwa ajili
ya kutengeneza madawati kabla ya muda wa
ukomo. Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri
hiyo ya Nzega, Emanueli Kitundu, alisema
Januari mwaku huu kulikuwa na upungufu wa
madawati 40,000, lakini mwezi huu upungufu ni
madawati 10,000.
Wahisani waokoa jahazi Miongoni mwa maeneo
ambayo wahisani mbalimbali wamejitolea kuokoa
jahazi la upatikanaji madawati ni mkoani
Manyara, ambao ni moja ya mikoa 19
inayopakana na hifadhi 16 za taifa, iliyopokea
fedha kutoka Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa)
. Tanapa ilitoa madawati 16,500 yenye thamani
ya Sh bilioni moja kuunga mkono mkakati wa
serikali. Hundi za fedha hizo zilitolewa kwa
wakuu wa mikoa 19 mkoani Arusha mbele ya
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.
Madawati hayo yatasambazwa katika shule za
msingi za wilaya 55 zinazopakana na hifadhi
hizo. Vile vile hivi karibuni, kampuni za Tanzania
Bundu Safaris na Rungwa Game Safaris,
zilikabidhi madawati 90 kwa shule ya msingi
Loiborsiret wilayani Simanjiro. Akipokea
madawati hayo juzi, Mkuu wa Wilaya ya
Simanjiro, Mahmoud Kambona, alishukuru
kampuni hizo na kusema huu ni wakati wa jamii
ya wafugaji kupata elimu.
Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro pia
imepata wahisani wakiwemo Ubalozi wa Japan,
ambao wamewatengenezea madawati 212 .
Akitoa taarifa hivi karibuni kwa Mkuu wa Mkoa
wa Morogoro, Dk Kebwe Steven, Mkurugenzi wa
Manispaa hiyo, Theresia Mahongo alisema
wamejipanga kukamilisha utengenezaji wa
madawati 6,672 kabla ya Juni 30, mwaka huu.
Alisema mahitaji ya madawati katika shule za
msingi ni 16,244, yaliyopo ni 12, 572 na upungufu
ni madawati 6,672 sawa na asilimia 34. “
Tumepata wahisani wa kututengenezea madawati
212 kutoka Ubalozi wa Japan na wengine ili
kukamilisha madawati,” alisema Mahongo. Vile
vile manispaa imepata kibali cha kuvuna miti
sita, itakayowezesha kupasua mbao 9,000
zitakazotengeneza madawati 300.
Aidha alisema pia imetengwa bajeti ya fedha kwa
ajili ya madawati. Manispaa ya Moshi Mkurugenzi
wa Manispaa ya Moshi mkoa wa Kilimanjaro,
Jeshi Lupembe alisema halmashauri imetenga Sh
milioni 20 zitakazotengeneza madawati 500 na
kufanya madawati yaliyotengenezwa na
halmashauri kuwa 750 na yaliyobaki 600
yatatolewa na wadau mbalimbali.
Alisema wadau mbalimbali waliojitokeza kusaidia
kuchangia madawati na idadi kwenye mabano ni
Kampuni ya vinywaji baridi ya Bonite, walioahidi
kutoa madawati 100, Benki ya Ushirika Mkoa wa
Kilimanjaro-KCBL (100), Chama cha Walimu na
Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa
madawati 20 na wadau wengine.
Alisema halmashauri imeshatoa Sh milioni 10 na
kuomba kibali cha kukata miti mitano kwa ajili ya
utengenezaji wa madawati 250 na vitanda 150
katika shule ya Moshi ufundi ambayo ndiyo
ilikuwa na upungufu mkubwa.
Dar yaandaa uchangishaji
Kwa upande wa Mkoa wa Dar es Salaam, Ofisa
Elimu wa Mkoa , Raymond Mapunda alisema
mkoa huo umejitahidi kupunguza uhaba wa
madawati kwa kushirikiana na wadau mbalimbali,
ingawa bado upo upungufu.
Alisema ili kumaliza tatizo hilo, wako kwenye
maandalizi ya mwisho ya kualika wadau kwenye
chakula cha jioni, hafla iliyopangwa kuzinduliwa
kati ya Juni 2 na 3 mwaka huu ili kuwashirikisha
wadau na wahisani mbalimbali.
“Kama mkoa tuna mambo makubwa matatu
tunayafanya ili kuhakikisha tunamaliza tatizo la
miundombinu ya elimu hasa kwa upande wa
madawati na vyumba vya madarasa, na jambo
mojawapo ni hilo la kuzindua uchangiaji wa vitu
hivyo kupitia chakula cha jioni tunachoandaa”,
alisema Mapunda.
Alisema mkoa una upungufu wa madawati 94,030
kwa shule za msingi na sekondari. Kwa upande
wa vyumba vya madarasa, kuna upungufu wa
vyumba 8,317. Akichanganua, Mapunda alisema
katika shule za msingi, madawati yaliyopo ni
102,175 na upungufu ni 66,301 huku upande wa
sekondari kuna viti na meza 99,189 na upungufu
ni viti na meza 27,729.
Hata hivyo alisema mwitikio wa wadau kuchangia
miundombinu hiyo ni mkubwa. Hivi karibuni
Umoja wa watoa huduma ya usafiri wa daladala
jijini hapo, wameahidi kuchangia madawati 100.
Mgawanyo huo ni kama ifuatavyo, wilaya ya Ilala
wamepata Sh milioni 323, Temeke, 391 na
Kinondoni 391. Halmashauri zenyewe zimetakiwa
kujitengea fedha kutoka vyanzo vyao kwa ajili ya
kununua madawati.
Wananchi wachangishana Mkoani Simiyu, wakazi
wa kijiji cha Luguru wilayani Itilima, katika
kuunga mkono mkakati huo, wameamua
kuchangishana Sh 10,000 kila kaya kwa ajili ya
kutengeneza madawati 380 ya shule ya msingi
kijijini hapo.
Mwenyekiti wa kijiji, Dolnad Aloyce alisema
waliwahamasisha wananchi kupitia mkutano wa
hadhara kwa ajili ya kufanikisha lengo hilo. Kwa
upande wa Wilaya ya Bariadi, Katibu Tawala wa
Wilaya ya Bariadi, Albert Rutahiwa, alisema
“Tumebakiza siku 42 (sasa 39) kukabidhi
madawati , hivyo wote kwa ujumla wetu jukumu
letu ni moja tuhakikishe upatikanaji wa mawadati
ifikapo Juni 30’’.
Taarifa kutoka mkoa wa Pwani, zinasema wilaya
ya Mkuranga hadi sasa, imefanikiwa kutengeneza
madawati 5,043 kwa ajili ya shule za msingi na
sekondari. Mkuu wa wilaya ya Mkuranga, Abdalla
Kihato alitoa taarifa hiyo kwa Mkuu wa Mkoa wa
Pwani, Evarist Ndikilo aliyekuwa ziarani humo.
Kihato alimhakikishia Mkuu wa Mkoa kwamba
hadi Juni 30, hawana wasiwasi tatizo la
wanafunzi kukaa chini litakuwa limekwisha kwani
wanashirikiana na wadau mbalimbali kutengeneza
madawati. Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa huo
wa Pwani, Ndikilo mkoa huo ulikuwa una
upungufu wa madawati 43,047 kwa shule za
msingi lakini kwa jitihada zilizopo, tatizo
limepungua kwa kiwango kikubwa.
Vile vile, Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Chiku
Galawa ameuhakikishia umma kuwa tatizo la
uhaba wa dawati kwenye halmashauri zilizopo
mkoani kwake litamalizika kabla ya Juni 30.
Alisema kwa mkoa mzima wa Songwe mahitaji
ya madawati ni 63,537 ambapo yaliyopo ni 49,692
hivyo pungufu ni madawati 11,804.
Imeandikwa na Lucas Raphael, Igunga, John
Gagarini, Kibaha, Joachim Nyambo, Mbozi,
Kareny Masasy, Itilima, John Nditi, Morogoro,
Ikunda Erick, Dar es Salaam na Arnold Swai.chanzo habar leo.
Moshi

Watunishi hewa wayaponza mabenki.soma zaid

Watunishi hewa wayaponza mabenki.soma zaid


MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul
Makonda ametoa siku 21 kwa benki zilizokuwa
zikitumika kuweka mishahara ya watumishi hewa,
kurejesha fedha hizo serikalini ; au kubainisha
waliokuwa wakitumia akaunti hizo, kuchukua
fedha.
Akizungumza na waandishi wa habari jana,
Makonda alisema benki ndio pekee wanaoweza
kusaidia mkoa, kutambua wahusika waliokuwa
wanatumia akaunti hizo pamoja na wale
waliokuwa wanachukua fedha hizo.
Alisema watu hao wasipopatikana, inamaanisha
fedha bado zipo katika benki hizo, hivyo
zinapaswa kuzirudisha serikalini zifanye
maendeleo kwa wananchi. “Tayari
tumeshaziandikia benki hizo barua na kuwapatia
majina na akaunti na kuwataka kutuwasilishia
majina ya wahusika, waliohusika na akaunti hizo
ili kusaidia kutambua mtandao mzima wa
wahusika wa suala la watumishi hewa ambao
wameigharimu serikali,” alisema Makonda.
Alitaja benki hizo pamoja na fedha wanazodai
kuwa ni benki ya NMB ambayo inadaiwa zaidi ya
Sh bilioni mbili, CRDB zaidi ya milioni 400, NBC
zaidi ya milioni 141, DCB milioni 85, Standard
Chartered zaidi ya Sh milioni mbili na Community
Benki zaidi ya milioni 100.
“Hakuna mtu anayeweza kutumia akaunti ya mtu
bila kufuata taratibu za kibenki, hata kama mtu
amefariki kuna taratibu za kufuata ndipo apate
akaunti, naamini benki hizi zitasaidia
kuwatambua wahusika wote,” alisisitiza.
Aidha, alizitaka benki hizo kufunga huduma za
akaunti hizo ;na zisifanye malipo yoyote mpaka
fedha hizo zitakapopatikana. Mpaka sasa, Mkoa
wa Dar es Salaam umebainika kuwa na
watumishi hewa 283, ambao wanadaiwa
kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 3.6
ambazo zilitumika kuwalipa mishahara.

Saturday, May 21, 2016
Mvua kubwa iliyonyesha imesababisha vifo vya watu 70 huko sri Lanka.soma zaid.

Mvua kubwa iliyonyesha imesababisha vifo vya watu 70 huko sri Lanka.soma zaid.

Utawala nchini Sri Lanka unasema kuwa
zaidi ya watu 70 sasa wanafahamika
kuaga dunia kwenye maporomoko ya
udongo yaliyosababishwa na mvua
kubwa.
Zaidi ya watu wengine 120 bado
hawajulikani waliko.
Katika maeneo mengine ya mji mkuu
Colombo, maji yalipungua kwa kiasi leo
Jumamosi lakini kwenye sehemu zingine
maelfu ya watu waliolazimika kuhama
kutokna na mafuriko na maporomoko ya
Udongo bado wanaishi kwenye makao ya
muda.
Misaada ya dharura yakiwemo mahema na
mashua sasa vinawazili kutoka nchini
India.

Sura 4 za Raisi john magufuli kumtumbua kitwanga.soma zaid.

Sura 4 za Raisi john magufuli kumtumbua kitwanga.soma zaid.

JAMII ya Watanzania imetakiwa kujifunza sura
za Rais John Magufuli, kutokana na hatua yake
ya kutengua uteuzi wa aliyekuwa Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga.
Akizungumza na gazeti hili jana kuhusu hatua
hiyo ya Rais Magufuli, Mwenyekiti wa Jumuiya
ya Wafanyabiashara Tanzania, Johnson Minja,
alisema Rais ametuma salamu kwa sura nne
kupitia utenguzi huo.
Sura ya kwanza kwa mujibu wa Minja, alisema
Rais amewakumbusha watumishi wote wa umma
kwamba uadilifu ni jambo muhimu mahali pa kazi,
na wanapaswa kuheshimu na kutekeleza
majukumu yao kwa kuzingatia muda na sio
kutumia muda huo vibaya.
Pili, Minja alisema Rais ametuma salamu kwa
walio karibu yake, kwamba uswahiba wao
hauhusiani na kazi ya nchi, hivyo suala la
kufahamiana si kigezo cha kiongozi avunjaye
maadili kuachwa, bali wanapaswa kutambua nchi
inaongozwa kwa Sheria na Katiba.
Akizungumzia sura ya tatu ya uamuzi huo, Minja
alisema Rais amewakumbusha Watanzania kuwa
haangalii muda gani amemteua kiongozi au muda
gani ametumikia nafasi aliyopewa, bali
kinachoangaliwa ni utendaji kazi wake kwa Taifa.
Aidha sura ya nne, imeelezwa kwamba Rais
ameoneshwa kuwa haendeshwi kwa siasa za
vyama kwa kuangalia wanasiasa watasema nini,
hasa wakati huu wa uwepo wa Sakata la
Kampuni ya Lugumi, na kusema alichoangalia ni
kosa limetendeka muda gani.
“Kwa kweli Rais kaonesha ukomavu wake,
ameonesha ni Rais mwenye msimamo, bila kusita
amefanya uamuzi sahihi, hakuangalia vyama vya
siasa vinasema nini, bali aliangalia maadili ya
utumishi wa umma yanasema nini na kuchukua
hatua,” alisema Minja.
Watumishi wengine
Kwa upande wake Profesa wa Chuo Kikuu cha
Dar es Salaam na mchambuzi wa habari, Kitila
Mkumbo, alisema uamuzi huo wa Rais ni hatua
muhimu, na amefanya jambo kubwa na sahihi
hivyo mawaziri wengine wanapaswa kuwa
makini.
“Ni hatua kubwa, Rais amefanikiwa kuvuka hili,
ameonesha uwezo wake wa kufanya uamuzi na
sio kuangalia sura kwa minajili ya urafiki, au
kufahamiana, ukiwa kiongozi unapaswa
kujitambua hadhi yako na nafasi yako kwa jamii,”
alisema Profesa Mkumbo.
Alisema hatua hiyo imesaidia Rais kuondokana
na lawama ya Sakata la Kampuni ya Lugumi na
inaashiria kwamba taasisi nyingine za Serikali
zitafanya kazi zake mapema badala ya kumsubiri
Rais afanye kila kitu.
Profesa Mkumbo alitoa mfano kwenye utenguzi
huo na kusema Bunge lilikuwa na uwezo wa
kumzuia asiingie ndani ya ukumbi ule kwa hali
yake ya ulevi, ili asiiaibishe Serikali kama
ambavyo imeonekana, lakini hawakuchukua hatua
hadi Rais alipochukua.
“Sasa ni wazi kwamba Sheria za Kazi na Vileo
maeneo ya kazi zitaanza kufanya kazi, ili kila
mtumishi ajitambue na kufahamu wajibu aliopewa
ni dhamana na anatakiwa kutekeleza kwa
kuzingatia maadili,” alisema Profesa Mkumbo.
Jimboni nako watengue
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam (UDSM), Dk Benson Bana alisema
Kitwanga ameachishwa kazi kwa fedheha na
hata wapigakura wake kama sheria ingeruhusu
wangemwajibisha.
Alisema cheo ni dhamana na kwamba katika
nafasi aliyokuwa nayo ndani ya Baraza la
Mawaziri tena kwenye wizara nyeti, alipaswa
kuwa mfano wa kiongozi mwenye uadilifu na
haiba yake ifanane na hicho chombo.
“Rais katuma salamu nzito kwa wengine na
taasisi za umma, imetufundisha kuwa Rais
akikupa wadhifa, usimuangushe, huyu
kamuangusha Rais na Serikali, alipaswa
kuwajibishwa na amewajibishwa kwa wakati, bila
kushinikizwa,” alisema Dk Bana.
Alisema wananchi wanapaswa kumuelewa Rais
na kuacha kuzungumza maneno yasiyo na maana
kwani Kitwanga alipaswa kuwajibishwa kwa kosa
alilotenda kwa wakati huo la ulevi na Rais
amechukua hatua.
Dk Bana alisema kwa hatua hiyo ya Rais, ni wazi
kwamba wale wote wenye wadhifa katika
utumishi wa umma, wanapaswa kuheshimu na
kuzingatia misingi ya Maadili ya Utumishi wa
Umma na kama misingi hiyo huwezi kuitekeleza,
ni bora waache kazi mwenyewe.
Misingi ya Nyerere
Kwa upande wake Mhadhiri mwingine wa Chuo
hicho, Dk Bashiru Ally, alizungumzia suala hilo
kwa kurejea misingi ya Baba wa Taifa, Mwalimu
Julius Nyerere kuwa katika mambo muhimu
aliyoyajenga ni misingi ya utaifa na maadili ya
utaifa.
Alisema kiongozi ni hadhi na ni nafasi ya
heshima na kila kiongozi awe wa ngazi yoyote
kuanzia Serikali za Mitaa hadi urais, anapaswa
kutambua kuwa cheo ni dhamana na kina
masharti na maadili yake.
“Ni mara ya kwanza kwa rais kuonesha ukali,
ulevi ni jambo baya, linatakiwa kukemewa kwa
nguvu zote, ujumbe huu uende kwa taasisi zote
serikalini na kwa umma, pia walevi popote walipo
hizi salamu ziwafikie,” alisema Dk Bushiru.
Alisema kosa alilofanya Kitwanga lipo kwa
watumishi wengi wa umma na kwamba kwa
hatua hizo za Rais, Katibu Mkuu Kiongozi
anapaswa kupeleka salamu kwa taasisi zilizo
chini yake kuwakumbusha kwamba utumishi wa
umma unakwenda sambamba na maadili.
Swali kurudiwa
Kutoka bungeni, kitendo cha Kitwanga kujibu
swali akiwa mlevi, kimesababisha Serikali
kutakiwa kujibu upya swali hilo bungeni, huku
akimkasirisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Aidha, imefahamika kuwa watu wengi
‘walishitukia’ kuwa mbunge huyo wa Misungwi
mkoani Mwanza hakuwa ‘sawasawa’ wakati
akijibu swali bungeni Ijumaa asubuhi mjini hapa.
Uteuzi wa Kitwanga kwa wadhifa wa Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi umetenguliwa na Rais
John Magufuli juzi baada ya kubainika kuwa
waziri huyo aliingia bungeni na kujibu swali
linalohusu wizara yake akiwa amelewa.
Taarifa ya Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano,
Ikulu, Gerson Msigwa juzi kuhusu kutenguliwa
uteuzi huo wa Kitwanga ilikuwa na aya mbili tu.
“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk
John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa
Charles Kitwanga kuanzia leo tarehe 20, Mei,
2016. “Rais Magufuli ametengua uteuzi huo
kufuatia kitendo cha Mheshimiwa Charles
Kitwanga kuingia bungeni na kujibu swali
linaloihusu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
akiwa amelewa,” ilisema taarifa ya Kurugenzi ya
Mawasiliano, Ikulu.
Hali ilivyokuwa
Awali asubuhi, Kitwanga akijibu swali la Mbunge
wa Viti Maalumu, Devotha Minja (Chadema)
ambalo liliulizwa kwa niaba yake na Mbunge wa
Mlimba, Suzan Kiwanga (Chadema). Katika swali
la nyongeza, Kiwanga alihoji Wilaya ya Kilombero
ina miaka 55 lakini polisi hawana nyumba
wamepanga na Jimbo la Mlimba wanaishi
kwenye nyumba za Tazara, hivyo serikali ipewe
miaka mingapi kujenga nyumba na vituo vya
polisi.
Kitwanga alijibu: “Kwani wewe una miaka
mingapi? Usiulize miaka ya kujenga nyumba za
Polisi na vituo. Amini tutajenga tu. Halafu wewe
ni rafiki yangu lazima nikujibu hivyo.” Hata hivyo,
majibu hayo na jinsi alivyokuwa akijibu,
yaliwashitua wengi wakiwamo waandishi wa
habari ambao hawakumwelewa vizuri Kitwanga.
“Hivi mbona Kitwanga leo yuko hivi? Yuko sawa
sawa kweli,” alihoji mwandishi mmoja wa habari.
Hata wakati wa jioni kabla ya baadaye
kutangazwa taarifa za kutenguliwa kwa wadhifa
wa Kitwanga, mwandishi mwingine ambaye
hakuwamo ndani ya ukumbi wakati Kitwanga
anajibu maswali, aliuza: “Jamani hivi asubuhi
wakati Kitwanga anajibu maswali alikuwaje.”
Alijibiwa na wenzake kwamba hakuonekana kuwa
sawasawa, na mwingine akaenda mbali zaidi na
kueleza kwa alionekana amelewa. Waziri huyo
alitembelewa na wapigakura wake kutoka jimboni
na walitambulishwa miongoni mwa wageni
waliofika bungeni juzi.
Kuitwa na Waziri Mkuu
Lakini baada ya hali hiyo kutokea, inaelezwa
kuwa baada ya kipindi cha Maswali na Majibu
Bungeni, Kitwanga aliitwa ofisini kwa Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa ambaye awali alikuwamo
bungeni.
Inaelezwa Waziri Mkuu alikuwa amekasirika sana
kutokana na kilichofanywa na waziri huyo na
hakuwa yule aliyezoeleka miongoni mwa watu
wake.
Kilichoendelea kati yao hakikufahamika, lakini
kuna kila dalili alizungumza na Dk Magufuli
kutokana na kitendo cha uvunjifu wa maadili ya
utumishi kilichofanywa na Kitwanga, na
kusababisha rais kutengua uteuzi wake.
Katika taarifa yake juzi usiku saa chache baada
ya kutimuliwa Kitwanga, Waziri Mkuu Majaliwa
alisema uamuzi uliofanywa na Dk Magufuli
umefuata kanuni za utumishi wa umma ambao
unakataza mtumishi kulewa akiwa kazini.
“Zipo sheria za utumishi ambazo mtumishi
hatakiwi kunywa pombe na wala hapaswi kulewa
akiwa kazini… mtumishi anapaswa kuwa na akili
timamu inamwezesha kufanya kazi za Serikali,”
alisema Majaliwa akijibu swali la mwandishi wa
TBC1 aliyetaka kujua ukweli wa taarifa za
kutimuliwa Kitwanga. “Ni kweli Mheshimiwa Rais,
Dk John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mheshimiwa Charles
Kitwanga kuanzia leo tarehe 20 Mei, 2016 baada
ya kuonekana amelewa wakati wa kazi. Na hili
lilibainika pale alipokuwa akijibu maswali ya
wizara yake leo asubuhi,” alisema Waziri Mkuu.
Aidha, kutokana na majibu ya Kitwanga
kutoridhisha, Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini
(Chadema) aliomba mwongozo wa Spika kwamba
swali la Minja halikujibiwa kwa ukamilifu.
Kwa kawaida, maswali bungeni hujibiwa na naibu
mawaziri kwa kila wizara, na endapo wizara
haina naibu, hujibiwa na waziri husika. Na
endapo wote hawapo, huteuliwa naibu waziri
mwingine kujibu.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
Hamad Yussuf Masauni hakuwapo bungeni juzi
na imefahamika kuwa yuko safarini kikazi katika
moja ya mikoa nchini. Kwa mujibu wa Naibu
Spika Dk Tulia Ackson, swali la Minja lilikuwa:
“Askari wa Jeshi la Polisi na Magereza wanaishi
katika nyumba chakavu zisizokuwa na hadhi,
ikilinganishwa na kazi zao wanazozifanya kwa
jamii? Je, serikali ina mpango gani wa
kuwaboreshe askari makazi.”
Akitoa majibu ya mwongozo huo juzi usiku kabla
ya kuahirisha Bunge, Dk Ackson alisema
ilibainika kuwa si kwamba swali la Minja
halikujibiwa kikamilifu na Waziri, ila majibu yake
hayakutoa mchanganuo wa nyumba ngapi
zitajengwa kwa upande wa askari wa Jeshi la
Magereza.
“Kwa kuzingatia Mwongozo ulioombwa na
Mheshimiwa Mbunge, na uzito wa swali
lililoulizwa kiti kimeamua kuelekeza swali hilo
lirudiwe kuulizwa katika kikao cha tarehe 23 Mei,
2016. “Ili serikali iweze kutoa majibu kwa
ufasaha zaidi ikiwa ni pamoja na kutoa
mchanganuo wa nyumba ngapi za Askari
Magereza zitajengwa, na katika maeneo gani,”
alisema Naibu Spika.
Kitwanga aliyewahi kuwa Naibu Waziri wa
Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Ofisi ya
Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) na
Nishati na Madini anakuwa waziri wa kwanza
kutimuliwa katika Serikali ya Awamu ya Tano.
Mapema wiki hii, akifanya majumuisho ya hotuba
yake ya Bajeti kwa mwaka wa fedha 2016/17,
alisema yeye anatambulika kwa jina la ‘Bwana
STK.’ “Niko serikalini kwa miaka 35 sasa.
Natambulika kama Mr STK, Mzee wa STK –
Sheria, Taratibu na Kanuni.
Nimewasilisha fomu yangu Sekretarieti ya Maadili
kwa mara ya kwanza mwaka 1998. “Hivyo
vinatosha kuwapa taarifa mimi ni mtu wa aina
gani, sipendi kusema, napenda kutenda,” alisema
Kitwanga ambaye amekuwa akitajwa kuwa
mmoja wa marafiki wa karibu wa Dk Magufuli.chanzo habar leo.

Mkuu wa mkoa aagiza kukamatwa kwa mkurugenzi mtendaji na muweka hazima na wafikishwe mahakamani.soma zaid.

Mkuu wa mkoa aagiza kukamatwa kwa mkurugenzi mtendaji na muweka hazima na wafikishwe mahakamani.soma zaid.


MKUU wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo
ameagiza polisi mkoani humo kuwakamata na
kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria aliyekuwa
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Simon
Mayeye na aliyekuwa Mweka Hazina, Emmanuel
Joramu ili waweze kuhojiwa kuhusu ubadhirifu
wa mamilioni ya fedha za serikali.
Mulongo ametoa agizo hilo juzi kwenye kikao cha
majumuhisho ya ziara yake aliyoifanya wilayani
Bunda na kuagiza kuwa watuhumiwa wote
wakabidhiwe kwa Taasisi ya Kupambana na
Kuzuia Rushwa (Takukuru) pamoja na Mkaguzi
na Mdhibiti Mkuu wa Fedha za Serikali (CAG).
Agizo hilo alilitoa kutokana na taarifa ya baraza
la madiwani iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa
Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Issack Mayela
inayohusu ubadhirifu huo wa mamilioni ya fedha
ambazo ni zaidi ya Sh bilioni 2.3, zikiwemo za
ulipaji fidia wananchi wa kijiji cha Tairo ili
kupisha eneo la uwekezaji (EPZ).
Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa watumishi
hao wa serikali ambao kwa sasa wamehamishiwa
katika halmashauri nyingine watafutwe popote
pale walipo na wakamatwe mara moja na
kuhojiwa na kisha kutoa maelezo yao polisi, ikiwa
ni pamoja na hatua za kinidhamu na za kisheria
kuchukuliwa dhidi yao.
“Huyo Mkurugenzi na Mweka Hazina ambao
wametajwa katika taarifa hizo watafutwe mahali
popote walipo na kisha kuhojiwa dhidi ya
ubadhirifu huo na hatua za kinidhamu na kisheria
zichukuliwe dhidi yao…kazi hii naikabidhi CAG na
Takukuru na waikamilishe ndani ya siku 14,”
alisema.

Back To Top