Breaking News
Loading...

Advert

MICHEZO

MICHEZO

BURUDANI

BURUDANI

SIASA & JAMII KWA UJUMLA

SIASA & JAMII KWA UJUMLA

Recent Post

Tuesday, July 26, 2016
Basi la UDA usiku wa kuamkia leo limegongana na Treni.soma zaid

Basi la UDA usiku wa kuamkia leo limegongana na Treni.soma zaid

Taarifa iliyotufikia hivi punde, inaeleza
kuwa Basi la UDA lenye namba za usajili T
696 CVP limegonga treni katika eneo la
Kamata Jijini Dar es Salaam usiku huu
wakati Basi hilo likotokea stendi ya
Gerezani Kariakoo kuelekea Mbagala,
inadaiwa kuna watu wamejeruhiwa katika
ajali hiyo huku wengine wakidhaniwa
kupoteza maisha. tutawaletea taarifa
kamili baada ya kuipata kutoka vyombo
vya Ulinzi wa Usalama jijini Dar es
salaam.
Muonekano wa Badi hilo baada ya
Kugonga treni.

Sunday, July 24, 2016
Hii ni taarifa kutoka NACTE kuhusu  mfumo wa udahili wa pamoja.soma zaid.

Hii ni taarifa kutoka NACTE kuhusu mfumo wa udahili wa pamoja.soma zaid.

Baraza linapenda kutoa taarifa kuwa
Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS)
umefunguliwa tena kuanzia tarehe 22 Julai
2016 ili kujaza nafasi za udahili zilizo wazi
baada ya Baraza kuchagua waombaji
udahili waliowasilisha maombi yao
kuanzia tarehe 4 Machi 2016 hadi tarehe 3
Juni 2016. Mwisho wa kuwasilisha maombi
ni tarehe 5 Agosti 2016 saa sita usiku.
Waombaji wapya na baadhi ya waombaji
walioshindwa kukamilisha maombi yao
kupitia mtandao ilipofika tarehe 3 Juni
2016, wanaarifiwa kuanza kuwasilisha
maombi ya udahili kupitia Mfumo wa
Udahili wa Pamoja (CAS) ili kujaza nafasi
zilizo wazi. Waombaji wanahimizwa
kutumia muda huu wa nyongeza ili
kuwasilisha maombi.
Baraza linapenda pia kuwaarifu waombaji
udahili na umma kwa ujumla kuwa vikao
vya Kamati za kuidhinisha majina ya
waombaji udahili kupitia Mfumo wa
Udahili wa Pamoja (CAS) vilipitisha
orodha ya majina ya wenye sifa za udahili
kulingana na nafasi za udahili kwa kila
kozi zitolewazo na vyuo husika kati ya
tarehe 18 Julai 2016 na 21 Julai 2016.
Majina ya waombaji waliochaguliwa kwa
kila kozi itolewayo na chuo husika
yamekabidhiwa vyuoni kupitia Mfumo wa
Udahili wa Pamoja (CAS). Waombaji
waliochaguliwa nao wamearifiwa kupitia
kurasa (profile) zao binafsi au
kwa kubofya hapa.
Waombaji ambao hawakuchaguliwa
wamejulishwa sababu zilizowafanya
wasichaguliwe kupitia kurasa (profile) zao
pia.
Kwa waombaji wa Shahada ya Kwanza
waliowasilisha maombi yao kupitia
NACTE, Baraza linapenda kuwaarifu
kuwa, mashauriano kati ya NACTE na
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU)
yanaendelea kufanyika ili kufanikisha
udahili wa waombaji wa kozi za Shahada
ya Kwanza kama Serikali ilivyoagiza.
Imetolewa na
Ofisi ya Katibu Mtendaji
NACTE

Kanisa la KKKT lasalimu amri lipo layari kurudisha sh.29 ml.soma zaid.

Kanisa la KKKT lasalimu amri lipo layari kurudisha sh.29 ml.soma zaid.

Arusha. Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania
(KKKT) la Mjini Kati, Dayosisi ya Kaskazini
mkoani Arusha, limesema lipo tayari kurudisha
Sh129 milioni ambazo zilitolewa na Serikali kwa
ajili ya mishahara ya madaktari katika Hospitali
ya Selian ambayo linaimiliki.
Hatua hiyo imekuja baada ya Taasisi ya Kuzuia
na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kuwahoji
baadhi ya watumishi wa kanisa hilo na
kuchukua baadhi ya mafaili kwa kile
kilichoelezwa kwamba wanachunguza
mishahara hewa.
Katibu wa Dayosisi hiyo, Samwel Saiguran
alisema juzi ofisini kwake kwamba wapo tayari
kurudisha kiwango hicho cha fedha kwa
utaratibu, kwani waliwalipa madaktari ambao
hawakuwa katika orodha ya watumishi wa
Serikali kwa nia njema kuokoa maisha ya
Watanzania.
Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Arusha,
Juventus Baitu alisema taasisi yake inafanya
uchunguzi kuhakiki watumishi hewa Hospitali ya
Selian inayomikiliwa na kanisa hilo lakini
hakutaka kuingia undani wa suala hilo.

Wanafunzi wakamatwa wakiwa katika nyumba ya kujiuza.soma zaid.

Wanafunzi wakamatwa wakiwa katika nyumba ya kujiuza.soma zaid.


Mkuu wa Wilaya ya Rombo, Agness
Hokororo kwa kushirikiana na mbunge wa
Rombo Selasini, wamevamia nyumba ya
wageni Mkuu Rombo iliyokuwa ikitumika
kama Danguro la wanafunzi wa sekondari.
Baada ya Mwenyekiti wa Kijiji na majirani
kukamata wanafunzi usiku wa kuamkia
juzi wakiwa na chumba cha kubadilishia
Nguo za shule.
Iliamuriwa meneja wa Guest hiyo
akamatwe na Afisa biashara achukue
hatua za haraka kuifunga Guest hiyo hadi
itakapo amuriwa vinginevyo.
Rombo inatatizo la mimba za wanafunzi
jambo ambalo Mh Agness amedhamiria
kulikomesha hasa Tabia ya wazazi
kumalizama nyumbani.
Mh Dc anaomba ushirikiano toka kwa
wananchi wote.
ROMBO -UMOJA NI USHIND

Tbs yaendelea kuongeza ufanisi wa huduma bora kwa kufungua ofsi katika mikoa hii.

Tbs yaendelea kuongeza ufanisi wa huduma bora kwa kufungua ofsi katika mikoa hii.


Katika jitihada zake za kuongeza ufanisi
na huduma bora, Shirika la Viwango
Tanzania (TBS) limefungua ofisi za kanda
katika mikoa ya Arusha, Mwanza na
Mbeya.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo,
Dkt. Egid Mubofu (pichani) amewaambia
waandishi wa habari jana jijini hapa kuwa
hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa
bidhaa zinazozalishwa au kuuzwa kwa
watanzania zinakuwa na ubora na
viwango vinavyotakiwa.
“Ofisi hizi zitafanya kazi kwa karibu na
wazalishaji viwandani ili wananchi
wapate bidhaa bora,” alisema na
kuongeza kuwa watendaji katika ofisi hizo
watakuwa wanafanya ukaguzi viwandani
na kushughulika na maombi ya
wazalishaji wapya.
Alisema ofisi ya mkoa wa Arusha
itahudumia mikoa ya kanda ya kaskazini
ikiwemo Manyara, Kilimanjaro, Tanga na
Arusha yenyewe; Ofisi ya Mwanza
itahudumia Kanda ya ziwa mikoa ya
Mara, Kagera, Shinyanga, Simiyu, Geita
na Mwanza yenyewe.
Ofisi ya Mbeya itahudumia mikoa ya
nyanda za juu Kusini ya Iringa, Songwe,
Ruvuma, Njombe na Mbeya yenyewe.
Dkt. Mubofu alisema kwa muda mrefu
wazalishaji wa bidhaa viwandani
walikuwa wakipata huduma makao makuu
ya shirika Dar es Salaam na hivyo
kusababisha ucheleweshaji wa huduma.
Alisema ofisi hizo zitafichua viwanda bubu
vinavyo zalisha bila kufuata utaratibu.
“Ilikuwa ni vigumu kwa shirika kugundua
uwepo wa viwanda bubu katika maeneo ya
mikoani na wilayani kwa urahisi kutokana
na umbali lakini sasa kazi itafanyika bila
kikwazo,”alisema.
Pia shirika limefungua ofisi mipakani
katika mipaka ya Mutukula, Kasumulo na
Tunduma. Awali ilisha fungua ofisi Holili,
Horohoro, Sirari, Namanga na Rusumo.
Alisema kwa upande wa bandari
wamefungua ofisi katika bandari ya
Mwanza na Mombasa na pia wamefungua
ofisi katika uwanja wa ndege wa kimataifa
wa Kilimanjaro (KIA).
“Ufunguzi wa ofisi za mipakani unalengo
la kupunguza miaya ya uingizaji holela wa
bidhaa hafifu katika soko la Tanzania
unaofanywa na wafanyabiashara wasio
waaminifu,” alisisitiza Dkt. Mabofu.
Akitoa mfano alisema ufunguzi wa ofisi
katika bandari ya Mwanza na Mombasa
utapunguza uingizaji bidhaa hafifu toka
nchi jirani za Kenya na Uganda.
Alisema shirika limejipanga vyema na
kuwataka wananchi kushirikiana na ofisi
za mamlaka nchini kufichua viwanda
vinavyozalisha na wafanyabiashara
wanaokiuka utaratibu.

Ahukumiwa jela miaka 20 kwa kukutwa na pembe za ndovu 300.soma zaid.

Ahukumiwa jela miaka 20 kwa kukutwa na pembe za ndovu 300.soma zaid.


A Kenyan court handed a 20-year prison
sentence to a man who was found
possessing more than 300 elephant tusks
in what’s seen as a landmark ruling in the
East African nation’s fight against
poaching.
Principal Magistrate Diana Mochache said
in her ruling late Friday that there was
sufficient circumstantial evidence to
convict Feisal Ali Mohammed, who was
on Interpol’s most-wanted list for crimes
against the environment. The ivory was
discovered in a warehouse in the port city
of Mombasa in 2014. Feisal escaped
arrest during the raid but was arrested
later that year in neighboring Tanzania.
Feisal’s lawyers said they would appeal
the sentence. Four other defendants were
acquitted.
Source: Bloomberg

Kuna msemo usemao mzigo mzito mpe mnyamwezi au msukuma.soma zaid.

Kuna msemo usemao mzigo mzito mpe mnyamwezi au msukuma.soma zaid.

VIGOGO mashuhuri wa Chadema waliowahi kuwa
mawaziri wakuu; Edward Lowassa na Frederick
Sumaye, jana waligeuka gumzo ndani ya Mkutano
Mkuu Maalumu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
wa kumchagua Rais John Magufuli, kuwa
Mwenyekiti wa tano wa chama hicho.
Gumzo hilo, lilianzishwa na Katibu Mkuu wa
zamani wa CCM, Yusuf Makamba, alimpomtaka
Askofu wa Kanisa la Ufufuko na Uzima, Josephat
Gwajima, asimpotoshe Magufuli ili yasije
yakampata ya Sumaye, ambaye sasa anachezea
mchangani Kibaha.
Sumaye mchangani
“Hata akina Sumaye hawakuunda vyama vyao.
Bado wanahangaika; na sasa Sumaye anacheza
mchangani Kibaha,” alisema Makamba.
Sumaye ambaye aliwahi kuwa mjumbe wa
Kamati Kuu na NEC ya CCM, kwa sasa anawania
uongozi wa Kanda ya Pwani katika Chadema.
Kabla ya kusema kuwa Sumaye anahangaika na
siasa za mchangani, Makamba alimtaka Gwajima
kuacha uongo na kusingizia viongozi wa CCM.
Makamba aliyepewa nafasi ya kumuombea kura
Rais John Magufuli kwa wajumbe wa Mkutano
Mkuu Maalumu wa CCM, alisema anamtia moyo
Magufuli asiogope kuongoza chama, kwani
hataongoza peke yake bali wapo wanachama
wengi watakaomsaidia kazi hiyo.
“Wewe siyo wa kwanza kukataa kazi hii. Hata
watangulizi wako Kikwete na Benjamin Mkapa
nao walifanya hivyo hivyo,“ alisema Makamba
ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa
(NEC).
Makamba alisema hata manabii na mitume
wengi, kama Haruni, Mussa, Yona au Yunus na
Yeremia walifanya vivyo hivyo, walipopewa
utume au unabii na Mungu, kwani waliogopa
kufanya kazi hizo lakini, alisema mara zote
Mungu aliwaagiza kuwa wasiogope kuwa manabii
na mitume, kwani atatia maneno kwenye vinywa
vyao.
Aidha, Makamba alitaka viongozi wa dini mfano
Askofu Gwajima, waache kumfitini Kikwete eti
kwamba alikuwa hataki kumpa uenyekiti
Magufuli.
“Askofu Gwajima alikuwa anasingizia kuwa
Jakaya kiongozi wetu mpendwa hataki kukupa
uenyekiti. Alikuwa akikuhimiza kuwa kama hataki
uunde chama chako. Huu ni uongo. Gwajima
amemaliza uongo wote,” alisema Makamba na
kumuomba Magufuli asisikilize uongo wa kiongozi
huyo wa kiroho.
Makamba alimtaka Askofu Gwajima atambue
kuwa hata baadhi ya wana-CCM waliojiengua
mwaka jana, hawakuunda vyama vyao badala
yake wameangukia pua.
Aliwataka wajumbe wa mkutano huo, kumpa kura
zote za ‘Ndiyo’ Rais Magufuli, kisha Makamba
akaanza kutumia uhodari wake wa misemo,
methali, mafumbo na aya za Biblia na Kurani
Tukufu.
“Mzigo wa chama ulikuwa umebebwa na Mkwere
Kikwete ambaye sasa anaondoka; na kwa kuwa
kuna msemo kuwa ‘mzigo mzito mpe Mnyamwezi
au Msukuma, nawaomba wajumbe wote sasa
mzigo wa chama tumpe Msukuma Magufuli,”
alisema na kauli yake hiyo ilishangiliwa na
wajumbe.
Lowassa na ufisadi
Akielezea aina ya kiongozi anayetoka CCM na
anayeingia, Makamba alisema kuwa anayetoka,
Kikwete ni mpiganaji wa ufisadi, kwa kuwa
alifikia hatua ya kumtosa rafiki yake Edward
Lowassa, kuwa hafai kuwa Rais kwa kuwa
anatuhumiwa kwa ufisadi.
Alisema kada wa chama hicho anayeingia baada
ya Kikwete, Dk Magufuli yeye ndiye muasisi wa
Mahakama ya Mafisadi, ambayo tayari
imeshaanzishwa kwa Sheria ya Bunge. Kwa
mujibu wa Makamba, Kikwete ni kiongozi
aliyepiga vita umasikini na anapoondoka,
anayeingia Dk Magufuli msimamo wake ni
asiyefanya kazi na asile.
Kumchinja Kobe
Naye mmoja wa vigogo wa Chadema aliyerejea
CCM, Fred Mpendazoe, alikuja na dhana ya
namna ya kumchinja kobe, akifananisha na
utaratibu uliotumika, kukata jina la Lowassa
katika majina 38 ya wagombea urais.
Mpendazoe alisema Kikwete alifanya ‘timing’
sana kushughulikia ufisadi ndani ya chama hicho,
kwa kuwa kati ya makada hao 38 waliokuwa
wakiwania urais, baadhi akiwemo Lowassa
walikuwa na tuhuma za ufisadi na kukatwa kwa
majina yao, kulifanyika kwa wakati sahihi.
Kuachana na nzi
Mpendazoe pia alisema Wasambaa
walimfundisha msemo mmoja kwamba, mtu
akitaka asifuatwe na nzi, anatakiwa atupe mzoga
na kuongeza kuwa, hatua ya wagombea wenye
tuhuma za rushwa kutupwa, CCM ilitupa kibudu.
Kwa mujibu wa Mpendazoe, kuhamia Chadema
kwa Lowassa, kulisababisha chama hicho na
Ukawa waliomuunga mkono, kupoteza ajenda,
kwa kuwa walimpokea mtu waliyezunguka nchi
nzima wakimtuhumu kwa ufisadi tena wakisema
wanao ushahidi.
“Walipompokea Lowassa, nikasema basi mchezo
umekwisha wamepoteza ajenda,” alisema
Mpendazoe huku akishangaa kitendo cha Ukawa
kudai demokrasia imekuwa ikibanwa.
Gia angani
Mpendazoe alisema anashangaa kusikia Magufuli
anabana demokrasia na kuhoji kati ya chama
kilichotangaza nafasi ya urais na kuruhusu
wagombea 38 kugombea, huku mchujo ukifanyika
hadharani na kilichompata mgombea kwenye
chopa (helikopta), ni kipi chenye demokrasia?
Akifafanua zaidi, Mpendazoe alisema Chadema
ilimpata mgombea wake angani ndani ya
helikopta, na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe
alipokwenda katika vikao, akasema chama hicho
kimebadilisha gia angani.
“Nilihoji iweje uamuzi huo ufanyike bila vikao,”
alisema na kuongeza kuwa kilichofanyika kilikuwa
sawa na biashara na kuhoji kwa nini chama
hicho kisisajiliwe Brela (Ofisi ya Msajili wa
Makampuni) ili kufanya biashara.
CCM B
Naye Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema
alihoji yeye kuitwa CCM B, baada ya Rais
Magufuli kumteua kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya
Parole na kusema inakuwaje yeye aliyetoka
katika chama hicho mwaka 1995, apewe jina hilo.
Alisema kama kupewa cheo na Magufuli, ndio
sababu ya kuitwa CCM B, basi hata Mbunge wa
Vunjo, James Mbatia, ambaye pia ni Mwenyekiti
wa NCCR-Mageuzi na Mwenyekiti Mwenza wa
Ukawa, ni CCM B kwa kuwa aliteuliwa kuwa
Mbunge na Rais Jakaya Kikwete.
Mrema alisema kama kuitwa kwake CCM B ni
kutokana na kutoka ndani ya CCM; basi Lowassa
na Sumaye ni CCM A, kwa kuwa wao wametoka
mwaka jana wakati yeye ametoka tangu 1995.
Haeleweki
Naye Magufuli alisema alimshangaa Rais
mstaafu Benjamini Mkapa, kwa kumteua mtu
mmoja kuwa Waziri Mkuu kwa miaka 10
mfululizo, wakati waliofanyakazi na Waziri Mkuu
huyo, akiwamo yeye waliona kuwa ni mtu
asiyeeleweka. Waziri Mkuu wa Mkapa, alikuwa
Frederick Sumaye.
Kauli hiyo ya Magufuli, ilitanguliwa na ya
Kikwete, ambaye alishangaa kuona mtu aliyewahi
kuwa Waziri Mkuu, sasa anagombea uenyekiti wa
Kanda.

Back To Top