Breaking News
Loading...

Advert

MICHEZO

MICHEZO

BURUDANI

BURUDANI

SIASA & JAMII KWA UJUMLA

SIASA & JAMII KWA UJUMLA

Recent Post

Tuesday, May 3, 2016
Majambazi wanne wameuwawa mkoani tanga.

Majambazi wanne wameuwawa mkoani tanga.

Watu wanne wanaosadikiwa kuwa majambazi
ambao wanadaiwa kuhusika katika matukio
mawili tofauti ya uhalifu ikiwemo kuua watu
watano kisha kupora fedha katika duka la bidhaa
mbalimbali jijini Tanga wameuawa na Polisi
katika majibizano ya risasi baina yao katika
Mapango ya amboni yaliyopo nje kidogo mwa jiji
hilo.
Kamanda wa Polisi mkoani Tanga Kamishna
Msaidizi wa Polisi nchini Leonard Paul amesema
jijini Tanga kuwa baada ya kuuawa majambazi
hayo yalikutwa yakiwa na silaha mbali mbali
ikiwemo risasi za silaha aina ya Shotgun
zipatazo 120 kofia maalum za kuvalia usoni
wakati wa uhalifu na silaha nyingi baridi
wanazotumia wakati wa uporaji.
Kamanda Paul amesema katika tukio la
majibizano ya risasi askari wawili waliojulikana
kwa majina ya PC Charles alipigwa bomu katika
Mapango ya Amboni na kujeruhiwa sehemu za
mwili wake pamoja na Inspekta Mwakisol
ambaye risasi ilimparasa sehemu za usoni wakati
walipokuwa wakijibizana kwa risasi.
Kufuatia hatua hiyo Mbunge wa jimbo la Tanga
Mussa Mbaruk amesifu jitihada za jeshi hilo na
kulitaka kuongeza jitihada za kuimarisha hali ya
amani na utulivu kwa sababu jiji la Tanga
linatarajiwa kupokea sehemu kubwa ya
wawekezaji kutoka nje ya nchi ambao
wamevutiwa na fursa zilizopo kwa ajili ya
kuwekeza katika sekta ya viwanda.chanzo itv

Wanafunzi wa shule za msingi kenya waanza kunufaika na kompyuta.soma zaid.

Wanafunzi wa shule za msingi kenya waanza kunufaika na kompyuta.soma zaid.

Wanafunzi wa darasa la kwanza katika shule za
msingi, 151, nchini Kenya wamepokea kompyuta
hizo siku ya Jumanne.
Usambazaji wa tablets hizo unahusisha
wanafunzi 11,570 wa darasa la kwanza katika
shule 151 zilizoteuliwa.
Katika kaunti ya Mombasa, wanafunzi wa shule
ya Upili ya Sparki wamekabidhiwa kompyuta hizo.
"Tumepokea 'tablets' 80, laptopu mbili
zitakazotumiwa na walimu pamoja na mashine
moja ya kifaa cha kuonyesha picha kwenye ukuta
kwa kutumia mwanga". Anasema mwalimu mkuu
wa shule ya msingi ya Sparki Alfred Nthiga.
'Tablets' hizo zinawawezesha kutafuta maelezo
kwenye mtandao wa 'google'.
Katika mkondo wa kwanza wa kutekeleza mradi
huo, takriban shule tatu katika kila kaunti,
wanafunzi watopokea 'tablets', huku walimu
wakikabidhiwa laptopu
Kila shule iliyoteuliwa kupata vifaa hivyo kote
nchini itawezeshwa kupata huduma za mitandao
kwa kutumia Wi-Fi.
Mradi huo utaigharimu serikali ya Kenya dola
milioni 170.
Mradi huo wa kuwapa wanafunzi wa darasa la
kwanza tarakilishi bila malipo ni miongoni mwa
ahadi kuu za uchaguzi ambazo serikali tawala ya
Jubilee ilitoa mwaka wa 2013.
Hata hivyo utekelezwaji wa mradi huu
umekwazwa na tetesi za ufisadi pamoja na kesi
nyingi mahakamani.
Ahadi ya serikali ya Jubilee ya kutoa laptopu kwa
kila mwanafunzi wa darasa la kwanza katika siku
100 za kwanza haikutimizwa na badala yake,
laptopu zikabadilishwa na vibao vya 'tablets'
Serikali ya Jubilee pia iliahidi kuwapa wanafunzi
wa shule za msingi maziwa bila malipo, ahadi
ambayo hadi sasa haijatimizwa.
Baadhi ya wakosoaji wanashikilia kuwa mradi huo
haufai kupewa kipau mbele ikizingatiwa matatizo
chungu nzima yanayoikumba sekta ya elimu;
ikiwemo migomo ya walimu wakidai nyongeza ya
mishahara na ukosefu wa nguvu za umeme
katika maeneo mengi ya mashinani nchini Kenya.

Sumaye aibuka na kusema maneno haya dhidi ya Rais maguful.soma zaid

Sumaye aibuka na kusema maneno haya dhidi ya Rais maguful.soma zaid

FREDERICK Sumaye, Waziri Mkuu Mstaafu
ameeleza kushangazwa na Serikali ya Rais John
Magufuli kupenda kusifiwa zaidi na kuchukia
kukosolewa,
Sumaye bila kumtaja jina Rais Magufuli
ameleza kushangazwa na hatua ya serikali
kuminya uhuru wa habari na kwamba,
kufanya hivyo kunalenga kuficha madudu
yanayofanywa na watendaji wake.
“Wapowatawala ambao hawapendi kusemwa
lakini wanapenda sana kusifiwa. Kiongozi
mwenye tabia ya udikteta hataki kusikia kingine
zaidi ya sifa zake tu.
“Huyo ni mtu hatari na katika nchi ya namna hiyo
hakuna uhuru wa habari wala uhuru wa kutoa
maoni kwa woga wa kupotezwa kusikojulikana,”
amesema Sumaye.
Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini
Dar es Salaam katika maadhimisho ya Siku ya
Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyoratibiwa na
Chama cha Waandishi wa Habri za Siasa
(TAPOREA), Sumaye amesema, serikali inakiuka
Katiba ya nchi.
Amesema, serikali yoyote inayopambana na
vyombo vya habari na kuminya uhuru wa kufanya
kazi zao huwa ina tatizo kwa upande wa
wanaotawala.
Akitolea mfano wa hatua ya serikali kuzuia
matangazo ya moja kwa moja ya bunge Sumaye
amesema, kwa kufanya hivyo serikali imevunja
Katiba.
“Unapoondoa matangazo ya moja kwa moja ya
vipindi vya Bunge, kwanza ni kuvunja katiba.
Ibara ya 18 (d) ya Katiba inasema, kila mtu ana
haki ya kupewa taarifa wakati wote.
“Kwa kuzuia Bunge kuoneshwa ‘live’ (moja kwa
moja) wewe serikali unataka kutoa taarifa ya
Bunge kwa wakati unaoutaka na kwa taarifa
unayoitaka wewe,” ameeleza Sumaye.
Kuhusu sababu iliyotolewa kwamba, matangazo
hayo yanatumia gharama ya Sh. 4 bilioni
amesema haina mashiko.
Sumaye amesema, hata kama matangazo hayo
yatarushwa na ofisi za bunge bado, gharama
zitaongezeka zaidi kwa sababu Bunge litahitaji
kununua mitambo pamoja na kuajiri wafanyakazi
wake.
Sumaye amesema, serikali yenye demokrasia ya
kweli lazima ikubali wananchi wake kutoa maoni.
“Serikali yoyote yenye utawala bora, ingependa
mambo yake inayoyafanya kwa ajili ya wananchi
wake mambo hayo yajulikane kwa wananchi hao.
“Ukiona serikali inaficha mambo yake lazima
kuna mambo wanayoyafanya ambayo hayafai na
wasingependa jamii ijue,” amesema Sumaye.
George Maziku, Mkurugenzi Mtendaji wa
TAPOREA amesema, ripoti ya hali ya uhuru wa
waandishi wa habari na uhuru wa vyombo vya
habari kimataifa, iliyotolewa na Shirika la
Waandishi wa Habari Wasio na Mipaka lenye
Makao Makuu yake nchini Ufaransa haipendezi.
Amesema, ripoti hiyo inaonesha kuwa, katika
miaka 10 iliyopita zaidi ya waandishi wa habari
800 kutoka mataifa mabalimbali duniani
wameuawa wakiwa wanatekeleza kazi zao.
“Kitisho kingine kwa uhuru wa vyombo vya habari
nchini ni utamaduni mpya ulioasisiwa na
kuimarishwa na watawala wa sasa na
kuvishinikiza vyombo vya habri kutomkosoa Rais
John Magufuli na serikali yake.
“Matokeo yake, vyombo vingi vya habari nchini
vimelazimika kuandika habari za kumfurahisha
Rais Magufuli,” amesema Maziku.chanzo mwanahalisonline

Leo ni siku ya maadhimisho ya uhuru wa habari wewe mdau unalipi la kuongeo juu ya uhuru wa habar.

Leo ni siku ya maadhimisho ya uhuru wa habari wewe mdau unalipi la kuongeo juu ya uhuru wa habar.


Leo ni siku ya Madhimisho wa Uhuru wa
Habari, maadhimisho ya Mwaka Huu
yanafanyika kitaifa mjini Mwanza, Waziri Nape
Mnauye, Mzee Reginald Mengi, Baraza la
Habari Tanzania, MCT, Tanzania Media
Foundation, TMF, Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania, TCRA, MISA TAN,
Shirika la Umoja wa Mataifa UN ... na
wengine wengi wako ndani ya nyumba.
Maadhimisho yameishaanza asubuhi hii,
andamana nami nikikuletea kile
kinachojiri, ila kama kuna mwana JF
mwingine, tusaidiane ku update.
Karibu.
Paskali.
=====
Anyazungumza sasa ni Pili Mtambalike
anawakilisha Baraza la Habari Tanzania,
Media Council of Tanzania, MCT,
ameikumbushia kauli mbia ya
maadhimisho haya kwa mwaka huu,
"Kupata habari ni haki yako, idai!"
===
Sasa hivi anazungumza Edda Sanga,
Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa
Habari Wanawake Tanzania, TAMWA.
===
Sasa anazungumza Mwenyekiti wa Chama
cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari,
MOAT, Dr. Reginald Mengi.
Mengi amekemea rushwa kwenye vyombo
vya habari, amesema zile bahasha ni
rushwa, hivyo wapokea bahasha ni
majipu!, watumbuliwe!.
Duu!.
===
Leo Tumemkumbuka Mwangosi!.
Tumesimama dakika moja for him.
======
Waziri Nape
Wanahabari fichueni maovu bila woga na
mtukosoe ili tuijenge Tanzania yetu kwa
pamoja!
Sote ni watanzania, tunaweza kukaa na
kuamua kwa pamoja kuhusu hili la Bunge
Live
Tunaweza kukaa mezani kuamua upya
kuona namna bora ya kuboresha suala
urushaji wa matangazo ya Bunge
Uamuzi wa kuanzisha studio ya Bunge ni
uamuzi uliopitishwa na Bunge lililopita
kabla hata sijawa mbunge
Tutatunga Sheria kwa kuzingatia Sera
iliyopo. Muswada ukipita, utafuta sheria
kandamizi kama ile ya 1976
Maoni ya wadau juu ya maboresho ya
Muswada wa Vyombo vya Habari
yatafanyiwa kazi. Tunatunga sheria kwa
ajili ya watu
Kuna sheria zinalalamikiwa kuwa na
mapungufu... Serikali itakaa chini
kuangalia namna ya kuzirekebisha!
Nawahakikishia, Tutalinda, kuutetea na
kuukuza Uhuru wa Vyombo vya Habari
Tanzania
Z

Sunday, May 1, 2016
Hivi mpaka wananchi wanatishia kuchoma nyumba za polisi polis tatizo ni nini? soma zaid.

Hivi mpaka wananchi wanatishia kuchoma nyumba za polisi polis tatizo ni nini? soma zaid.

Wananchi wa kijiji cha Mkomilo kata ya
Okaoni wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro
wametishia kuchoma moto nyumba za Polisi na
kufunga kituo cha polisi Okaoni kwa madai kuwa
askari waliopo katika kituo hicho wameshindwa
kukabiliana na matukio ya uhalifu na hivyo
kusababisha mwenyekiti wa kijiji hicho kuuawa
karibu na kituo hicho bila kupata msaada wa
polisi licha ya kupewa taarifa.chanzo itv.

Ijue idadi ya wanafunzi wanaokufa kwa ajali za barabarani kila mwaka hii ni kwa mjibu wa takwimu iliyotolewa.soma zaid.

Ijue idadi ya wanafunzi wanaokufa kwa ajali za barabarani kila mwaka hii ni kwa mjibu wa takwimu iliyotolewa.soma zaid.

Jeshi la polisi nchini limesema wanafunzi 78
nchini wamepoteza maisha kutokana na ajali za
barabara huku 181 wakijeruhiwa katika kipindi
cha mwaka 2015.
By Hadija Jumanne, Mwananchi hjumanne@
mwananchi.co.tz
Dar Es Salam. Jeshi la polisi nchini limesema
wanafunzi 78 nchini wamepoteza maisha
kutokana na ajali za barabara huku 181
wakijeruhiwa katika kipindi cha mwaka 2015.
Hayo aliyasema leo na Mnadhimu wa Kikosi cha
Usalama barabarani kutoka Makao Makuu,
Fortunatus Muslim wakati wa utoaji zawadi kwa
washindi wa shindano la uchoraji alama za
usalama barabarani.
Muslim alisema kati ya wanafunzi 78 waliofariki,
wavulana walikuwa 40 na wasichana 38, huku
majeruhi wakiwa 181 ambapo kati ya hao
wavulana walikuwa 81 na wa kike 81.
"Maeneo hatarishi ambayo yanaongoza kwa
kusababisha ajali za barabarani katika Jiji la Dar
Es Salaam ni Lumumba, Mnazi mmoja, Mikumi,
Mtambani, Boko, Bunju na Kongowe." Alisema
Muslim.
Mashindano hayo ambayo yaliandaliwa na
kampuni ya Puma Energy yalilenga kutoa elimu
kwa wanafunzi wa shule za msingi juu ya
utumiaji wa alama za usalama barabarani.
"Jeshi la Polisi kupitia kikosi cha usalama
barabarani limeendelea kutoa elimu kwa
wanafunzi, madereva na Jamii kwa ujumla juu ya
matumizi sahihi ya barabarani" aliongeza Muslim
Alisema wanafunzi walioshinda shindano la
uchoraji wa alama za usalama barabarani ni
Shaibu Abdalah kutoka shule ya msingi Gongo la
mboto, Abdallah Hussein kutoka Osterybay na
Christian Mathias kutoka Gongo la mboto.
Awali, Meneja wa kampuni ya Puma Enegy,
Philippe Corsaletti alisema lengo la mashindano
hayo ni kutoa elimu kwa wanafunzi kuhusiana na
matumizi sahihi ya barabarani.chanzo mwananch.

Maafisa elimu wa halmashauri sita mkoan mara wasimamishwa kazi .soma zaid.

Maafisa elimu wa halmashauri sita mkoan mara wasimamishwa kazi .soma zaid.

Mkuu wa mkoa wa Mara Bw.Magesa Mulongo
ameagiza kusimamishwa kazi mara moja kwa
maafisa elimu wa halmashauri sita za mkoa wa
Mara huku Wakurugenzi Watendaji wa
halmashauri hizo wakitakiwa kujieleza baada ya
kushindwa kutoa zawadi za watumishi bora wa
idara ya elimu kwa mwaka mmoja hadi miwili
hatua ambayo amesema inachangia kushusha ari
ya utendaji wa kazi kwa watumishi hao.
Mkuu huyo wa mkoa wa Mara Bw.Magesa
Mulongo,ametoa agizo hilo mjini Musoma katika
viwanja vya shule ya msingi ya Mkendo wakati
wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani
katika mkoa wa Mara na kuelezwa na baadhi ya
viongozi wa vyama vya wafanyakazi katika wilaya
hizo kuwa licha kuteuliwa kwa wafanyakazi bora
lakini halmashauri hizo katika kipindi cha mwaka
jana na mwaka huu zimeshindwa kutoa zawadi
kwa wateule wao.
Kwa upande wao baadhi ya viongozi wa vyama
vya wafanyakazi mkoani Mara wakizungumza
katika maadhimisho hao mbali na kulaani vitendo
vya unyanyasaji vinavyofanywa na baadhi ya
waajiri dhidi ya watumishi lakini pia wamelaani
vikali kitendo cha waajiri kuwakata fedha
watumishi wao kwa ajili ya kununulia
vitambulisho vya kazi.
Awali wafanyakazi hao wa idara mbali za serikali
na sekta binafsi mkoani Mara wamefanya
maandamano wakiwa na mabango yenye ujumbe
mbalimbali yakianzia uwanja wa Posta hadi
uwanja wa mkendo huku mkuu huyo wa mkuu wa
Mara akitumia nafasi hiyo pia kuwataka waajiri
wote kuanzia sasa kutenga kiasi cha fedha kama
zawadi kwa kila mfanyakazi bora anayeteuliwa
kutoka katika idara yake.chanzo itv.

Back To Top